More details

Uzinduzi wa maombi ya Kitaifa ( Tanzania National Prayer Breakfast)

Uzinduzi wa maombi ya Kitaifa ( Tanzania National Prayer Breakfast)ambayo yanafanyika hapa Dodoma Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Center yamezinduliwa na na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi,Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako. Katika hotuba yake amepongeza waandaaji wa Kongamano hili kwamba linawajenga vijana kimaandili, kiimani na kuwafanya vijana kuwa wazalendo katika Taifa letu. Kabla ya kutangaza kufunguliwa Kwa Kongamano hilo Waziri alikariri maneno ya Mungu kama ifuatavyo: 1Yohana 2:14b Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu. Mithali 20:29(a) "Fahari ya vijana ni nguvu zao....." Kongamano limeandaliwa na ushirikiano wa Viongozi wa Kikristo nchini kutoka TEC,CCT,CPCT na SDA kupitia Kingdom Leadership Network Tanzania.