More details

Kikao cha Kupitia Mwongozo wa USCF katika vyuo vya elimu ya kati na vya elimu ya juu

Kikao cha Kupitia Mwongozo wa USCF katika vyuo vya elimu ya kati na vya elimu ya juu kimefanyika leo katika ofisi ya CCT Dodoma. Kikao hiki kimeongozwa na Mkurugenzi wa Umisheni na Uinjilisti Mchg. David Kalinga na kuhudhuriwa na Mkurugenzi wa Utawala CCT, Godlisten Moshi na Viongozi kamati kuu ya USCF na baadhi ya walezi na Wahadhiri wa vyuo vikuu. Neno la kuongoza kikao limetoka kitabu cha 1Kor. 14:40 Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu