Mradi wa USAID Tuwajibike umefika Pwani mojawapo ya Mikoa 11 ambapo Mradi unatekelezwa ,na kufanikiwa kuzungumza na viongozi wa Serikali za Mtaa katika Kijiji cha Bungu pamoja na wananchi. Mradi wa USAID Tuwajibike unalenga Kuunga Mkono Jitihada za Serikali katika kuhimiza na kukuza uwajibikaji wa Serikali ,uwazi na kuongeza ushiriki wa jamii katika Kusimamia Rasilimali za Umma.
Baada ya mapokeo mazuri kwa kushirikiana na viongozi na wanachi wa kijiji cha Bungu ,walifanikiwa kuunda Kamati ya Ufualitiliaji wa Matumizi ya Rasilimali za Umma.
“Mapendekezo yangu nashauri mbeleni mradi unapoendelea kuweza kufikia vijiji vyote Saba, kulingana na uhitaji wa elimu ya usimamizi wa Rasilimali za Umma bado ni changamoto na Elimu hii iwe ni endelevu” - Diwani Bungu Ramadhan Mpendu