More details

Katibu Mkuu CCT ashiriki Mkutano wa Wachungaji wote wa KKKT-DODOMA

Katibu Mkuu CCT ashiriki Mkutano wa Wachungaji wote wa KKKT-DODOMA Mkutano wa tano (5) wa Wachungaji wote wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania unaendelea hapa katika ukumbi wa Chuo Kikuu Dodoma (UDOM) Jijini Dodoma. Mkutano ulianza tar 10 Septemba na utahitimishwa tar 15 Septemba 2022, ambapo zaidi ya wachungaji elfu mbili wameweza kusiriki. Katika Mkutano huu Katibu Mkuu wa Jumuitya ya Kikristo Tanzania Mchg. Dkt. Canon Moses Matonya leo tar 13 ametoa pongezi la washiriki kuitikia vizuri mkutano huo. Ambapo pia amewashukuru kwa kuwa KKKT ni Kanisa lenye mchango mkubwa katika kuinarisha umoja wa CCT. Pia amewashukuru kwa kuwa ni moja ya wachungaji wengi wanajitajidi sana kutoa elimu ya kiroho kwa watoto walioko shuleni kupita UKWATA na kwa wanafunzi walioko Vyuoni(USCF). Katibu Mkuu ameeleza kuwa miongini mwa vyanzo vya mapato katika kuimarusha CCT ni sadaka ya CCT Day na michango ya Uanachama, kanisa la KKKT limekuwa mfano mzuri katika kutekeleza hayo. Amewaomba wachungaji kuendelea kuimarisha Upendo wa Yesu Kristo, kwa kuwa tukiwa na Upendo, migogoro kwa Makanisa au familia na sehemu nyingine yoyote haitaweza kutokea. Ametoa wito tuendeleza kuimarisha umoja wetu wa CCT, kwa kuwa tukiwa wamoja tutakuwa na sauti ya pamoja. Ili kuimarisha hili tumeunda uongozi wa CCT Mikoani, hivyo tuutumie uongozi huo katika kuinarisha umoja wetu. Pia amesisitiza washiriki kuzifanya kazi zote kwa pamoja hasa katika kutoa elimu mashuleni na vyuoni ili kila shule au kila darasa liwe na mwalimu wa kiroho. Amehimiza wachungaji kushiriki kikamilifu siku ya CCT Day ili kuimarisha Zaidi chombo hiki. Ujumbe wakati wa Mkutano huu “Lichungeni Kundi la Mungu….” 1Petro 5:2